Ufunuo wa Yohana Mlango 8 Revelation

Ufunuo wa Yohana 8:1 Revelation 8:1

Hata alipoifungua muhuri ya saba, kukawa kimya mbinguni kama muda wa nusu saa.

Ufunuo wa Yohana 8:2 Revelation 8:2

Nami nikawaona wale malaika saba wasimamao mbele za Mungu, nao wakapewa baragumu saba.

Ufunuo wa Yohana 8:3 Revelation 8:3

Na malaika mwingine akaja akasimama mbele ya madhabahu, mwenye chetezo cha dhahabu, akapewa uvumba mwingi, ili autie pamoja na maombi ya watakatifu wote juu ya madhabahu ya dhahabu, iliyo mbele ya kiti cha enzi.

Ufunuo wa Yohana 8:4 Revelation 8:4

Na moshi wa ule uvumba ukapanda mbele za Mungu pamoja na maombi ya watakatifu, kutoka mkononi mwa malaika.

Ufunuo wa Yohana 8:5 Revelation 8:5

Na huyo malaika akakitwaa kile chetezo, akakijaza moto wa madhabahu, akautupa juu ya nchi, kukawa radi na sauti na umeme na tetemeko la nchi.

Ufunuo wa Yohana 8:6 Revelation 8:6

Na wale malaika saba wenye baragumu saba wakajifanya tayari ili wazipige.

Ufunuo wa Yohana 8:7 Revelation 8:7

Malaika wa kwanza akapiga baragumu, kukawa mvua ya mawe na moto vilivyotangamana na damu, vikatupwa juu ya nchi; theluthi ya nchi ikateketea, na theluthi ya miti ikateketea, na majani mabichi yote yakateketea.

Ufunuo wa Yohana 8:8 Revelation 8:8

Malaika wa pili akapiga baragumu, na kitu, mfano wa mlima mkubwa uwakao moto, kikatupwa katika bahari; theluthi ya bahari ikawa damu.

Ufunuo wa Yohana 8:9 Revelation 8:9

Wakafa theluthi ya viumbe vilivyomo baharini, vyenye uhai; theluthi ya merikebu zikaharibiwa.

Ufunuo wa Yohana 8:10 Revelation 8:10

Malaika wa tatu akapiga baragumu, nyota kubwa ikaanguka kutoka mbinguni, iliyokuwa ikiwaka kama taa, ikaanguka juu ya theluthi ya mito, na juu ya chemchemi za maji.

Ufunuo wa Yohana 8:11 Revelation 8:11

Na jina lake ile nyota yaitwa Pakanga; theluthi ya maji ikawa pakanga, na wanadamu wengi wakafa kwa maji hayo, kwa kuwa yalitiwa uchungu.

Ufunuo wa Yohana 8:12 Revelation 8:12

Malaika wa nne akapiga baragumu, theluthi ya jua ikapigwa, na theluthi ya mwezi, na theluthi ya nyota, ili kwamba ile theluthi itiwe giza, mchana usiangaze theluthi yake, wala usiku vivyo hivyo.

Ufunuo wa Yohana 8:13 Revelation 8:13

Kisha nikaona, nikasikia tai mmoja akiruka katikati ya mbingu, akisema kwa sauti kuu, Ole, ole, ole wao wakaao juu ya nchi! Kwa sababu ya sauti zisaliazo za baragumu za malaika watatu, walio tayari kupiga.